Stamina ameieleza fulltainment kuwa ameamua kuachia albam yake Mount Uluguru si kwasababu ya kutegemea apate fedha bali anataka kutengeneza profile ya mziki wake.
Akiongea na Fulltainment amesema
"Kumbuka kuna leo na kesho, leo upo kesho unapotea kwenye
muziki unadhan watu watakukumbuka
kwa lipi?? Lakini kama una albamu mashabiki watakukumbuka kwa kusikiliza kazi zako,kwahiyo albamu ni profile
ya msanii ila wasanii wengi wa bongo wanaangalia hela kupitia albamu.
Kwahiyo wadau wasubiri albam ya Mount uluguru itatoka na
nyimbo 23.nyimbo zangu zilizotoka lazima ziwepo kwenye albamu ndomaana watu
wengi hawajui kwann nyimbo zangu nilikuwa nazitoa kwa mfululizo namnaile.
Nyimbo utakazozisikia ni KABWELA,ALISEMA,NAJUTA KUBALEHE then
ipo WAZO LA LEO na KAMWAMBIE MWENZIO
then itakuja MGUU PANDE MGUU SAWA
Albam hiyo inatarajiwa kuzinduliwa jumamosi hii huko
morogoro may 30 na katika uzinduzi huo mgeni rasmi ni AFANDE SELE
No comments