ULE MSALA WA SHILOLE kuonekana nusu uchi akiwa kwenye stage ya show yake huko ubelgiji iliyofanyika mwezi uliopita hatimae umeisha na kufikia muafaka na basata leo.
Sakata hilo ambalo lilifika mpaka bungeni ambapo Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Bw Juma Nkamia alisema serikali ililiagiza Baraza La Sanaa la Taifa kufanya mazungumzo na Shilole ili Serikali iweze kuchukua hatua .
Basata ilifanya jitihada za kumtafta Shilole na kuongea nae leo na hatimae kumaliza na kufikia mahali pazuri. Shilole akiongea na Fulltainment leo ameielezea furaha yake baada ya kusamehewa na Basata alipoenda kutoa maelezo leo.
“Juzi Basata waliniita leo nimeenda kusikiliza wito wao,tumeongea mengi nashukuru wamenielewa na nafikiri kuanzia sasa hakuna tena tatizo kwasabu wale ni kama wazazi kwa mtoto wao wanatakiwa kumkanya yoyote aliekuwa ndani ya sanaa kama mtoto wao.
“Tumeelezana mengi kipi kifanyike na kipi kisifanyike katika sanaa ,Nimewaeleza kwa kirefu kile kilichotokea wamenielewa na wameniambia pia niwe muangalifu katika mavazi niwapo kwenye show zangu.”
PAMAOJA WADAU
ReplyDelete